MAOMBI YA KUJIUNGA NA MAFUNZO- 2022/2023
Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA) kupitia Kampasi za Tengeru, Buhuri, Mpwapwa, Morogoro, Madaba, Temeke, Mabuki na Kikulula- inakaribisha maombi ya kujiunga na mafunzo katika fani zinazohusu mifugo, katika mwaka wa masomo 2022/2023.
- Kozi zitolewazo ni;
- Astashahada na Stashahada ya Afya na Uzalishaji wa Mifugo.
- Astashahada na Stashahada ya Ufundi Sanifu wa Maabara ya Veterinari.
- Stashahada ya Uendelezaji wa Nyanda za Malisho na Udhibiti wa Ndorobo.
- Sifa za mwombaji
- Awe amehitimu Kidato cha Nne na kufaulu angalau masomo manne kwa alama D na kuendelea. Kati ya masomo hayo mawili yawe ya Sayansi ambayo ni Biolojia, Kilimo, Kemia, Fizikia, Hisabati na Jiografia
- AU
- Kidato cha Sita mwenye subsidiaries mbili za masomo ya sayansi,
- AU
- Mhitimu wa kidato cha nne na amejiendeleza katika vyuo vya ufundi VETA vyenye mkondo wa mifugo na kupata NVA Level 3 au Trade Test I.
Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 30/07/2022.
Wanafunzi waliochaguliwa na OR-TAMISEMI kujiunga na mafunzo katika kampasi za LITA mnakumbushwa kuthibitisha na kupakua fomu ya maelekezo ya kujiunga na mafunzo kupitia Tovuti ya LITA www.lita.go.tz
Kwa mawasiliano zaidi tumia namba zifuatazo: 0754 746 782; 0754 828 688; 0786 203 825 na 0733 540 544; AU tembelea Tovuti ya Wakala: www.lita.go.tz
WOTE MNAKARIBISHWA